President wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli katika picha ya pamoja na Makamu
wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa na Luteni
Mstaafu Chiku Gallawa baada ya kumuapisha kuwa mkuu wa mkoa mpya wa Songwe
Ikulu jijini Dar es salaam Machi 28, 2016.
Mkuu wa Mkoa wa Songwe Luten Mstaafu Chiku Galawa ameanza ziara ya kutembelea Wilaya zote tano za Mkoa huo.
Na Mdollo Timotheo M,
Mkuu wa Mkoa wa Songwe Luten Mstaafu Chiku
Galawa ameanza ziara ya kutembelea Wilaya zote tano za Mbozi Songwe,Ileje,Momba
na Songwe ambazo zinaunda Mkoa wa Songwe ili kujitambulisha kwa wananchi na
kupokea changamoto mbalimbali zinazozikabili wilaya hizo.
Galawa ameanza ziara katika Wilaya ya Songwe
ambapo alipokelewa katika Kijiji cha Kaloleni Kata ya Mkwajuni na Vijana
waendesha Bodaboda walioambatana na Mbunge wa Jimbo la Songwe Philip Mulugo
ambaye ni mlezi wa Vikundi mbalimbali vya waendesha pikipiki Wilaya ya Songwe.
Mkuu wa Mkoa Chiku Galawa alipokea changamoto
mbalimbali za Jimbo la Songwe kutoka kwa Mbunge wa Jimbo hilo ikiwa ni pamoja
maji,barabara,umeme na Afya.
Mulugo amesema kuwa wilaya hiyo mpya ina eneo la
kutosha kujenga nyumba za watumishi wa wilaya hiyo na ofisi mbalimbali pia
Asasi ikiwa ni pamoja na ujenzi wa Benki ya NMB ili kuwaondolea adha wakazi wa
Mkwajuni kutokana na kutokuwepo kwa Taasisi za kifedha.
Kwa upande wa Mkuu wa Mkoa kabla ya
kuwawahutubia wananchi katika uwanja wa michezo wa Mkwajuni alivikwa uchifu na
wazee wa kimila wa kabila la Kibungu wakiongezwa na Chifu Kazumba ambaye pia
alimkabidhi mbuzi mnyama kama ishara ya upendo na ukaribisho wilayani humo.
Akiwahutubia mamia ya wakazi wa Mkwajuni Galawa
amweshukuru wakazi wa Mkwajuni kwa maaribisho mazuri na kusema kuwa changamoto
zilizopo katika Mkoa wake mpya zitumikke kama fursa ya kuleta maendeleo katika
wilaya hiyo na Mkoa kwa ujumla.
Ameendelea na kusema
Wilaya ya Songwe ina ardhi nzuri,Ziwa
Rukwa na madini mbalimbali ambayo yatakuwa chachu ya maendeleo kama
Dhahabu,makaa ya mawe na madini adimu duniani yanayotumika kutengezea vifaa vya
elekroniki ambayo yanapatikana katika Kata ya Ngwala.
Galawa ataendelea na ziara yake katika wilaya za
Mbozi Momba,Ileje na Mbozi ambapo atakuwa na kazi ya kupokea kero kutoka kwa
wananchi na kuzipatia ufumbuzi ili kuleta maendeleo katika Mkoa wa Songwe.
Refference to Songwe yetu by Kamanga na Matukio